Skip to main content Accessibility help
×
Hostname: page-component-848d4c4894-tn8tq Total loading time: 0 Render date: 2024-06-23T09:28:16.451Z Has data issue: false hasContentIssue false

32 - Wasomi, Lugha za Ulaya na za Kiafrika: Kati ya Kuweza na Kuwezwa

from Part V - The Other Ngũgĩ

Published online by Cambridge University Press:  27 July 2019

Ngũgĩ wa Thiong'o
Affiliation:
Distinguished Professor of English and Comparative Literature at the University of California, Irvine.
Get access

Summary

(Mhadhara wa hadhara uliotolewa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ukumbi wa Nkrumah, baada ya kutunukiwa Digrii ya Heshima ya Uzamifu [PhD] na Chuo hicho, 23 Novemba, 2013)

Katika mhadhara huu, nataka kuangalia na kufafanua, kwa ufupi tu, uhusiano wa kitaaluma kati ya lugha za Afrika na za Ulaya, na hasa Kiingereza. Jambo hili ni muhimu katika wakati huu, ambapo nchi nyingi za Afrika zinasherehekea miaka hamsini tangu zipate uhuru wake kutoka utawala wa kikoloni.

Msomi, au mwanataaluma wa aina yoyote ile, si kitu kipya kwa Afrika: Kila jamii, za leo au za kale, zilikuwa na wasomi au wanataaluma wake. Tunalitumia hili neno ‘msomi’ kwa maana ya mtu anayeshughulika na fikira. Yawezekana kwamba msomi huyo huenda akawa ana ujuzi mwingine; lakini kazi yake kuu inayojitokeza ni matokeo ya kujishughulisha kwake na fikira. Katika kundi hili wanaingia pia waganga wa kimwili na wa kiroho, wahunzi (au wafua vyuma), wajenzi, na mafundi wengineo.

Watu kama hawa walikuwa ni miongoni mwa wajenzi wa utamaduni wa Misri, Uhabeshi, Zimbabwe, Songhai, na kwengineko. Kati ya hao, alikuwamo pia mshairi, ambaye alichanganya ujuzi wa historia, maadili na utabiri. Afrika ya Magharibi, mtu kama huyo aliitwa ‘griot’. Uswahilini kulikuwa na washairi wengi waliokuwa ni viongozi wa fikira, na ambao wameendelea kuweko karne baada ya karne. Kitabu alichokihariri Abdilatif Abdalla, na kuchapishwa na shirika la Mkuki na Nyota, kiitwacho Kale ya Washairi wa Pemba: Kamange na Sarahani, kina majina ya wachache kati ya hao. Miongoni mwao wakiwemo Fumo Liyongo wa Bauri (karne ya kumi na mbili); Zahidi Mgumi (karne ya kumi na nane); Muyaka bin Haji; Suud bin Said al-Maamiriy; Kamange na Sarahani (wote ni wa karne ya kumi na tisa); na wengineo walioishi katika karne ya ishirini. Washairi kama hawa walikuwa ni sauti za jamii zao, na pia watetezi wa haki. Ni muhimu kueleza hapa kwamba washairi-wasomi kama hao – tangu hizo zama za ustaarabu wa Misri, mpaka katika ustaarabu wa Waswahili – walitumia lugha za jamii zao. Yaani wasomi wa kabla ya kuvamiwa na utawala wa kikoloni, walikuwa wameshikamana na mizizi ya jamii zao.

Leo nataka kuzungumza, kwa ufupi tu, kuhusu msomi Mwafrika wa zama zetu.

Type
Chapter
Information
Ngugi
Reflections on his Life of Writing
, pp. 186 - 193
Publisher: Boydell & Brewer
Print publication year: 2018

Access options

Get access to the full version of this content by using one of the access options below. (Log in options will check for institutional or personal access. Content may require purchase if you do not have access.)

Save book to Kindle

To save this book to your Kindle, first ensure coreplatform@cambridge.org is added to your Approved Personal Document E-mail List under your Personal Document Settings on the Manage Your Content and Devices page of your Amazon account. Then enter the ‘name’ part of your Kindle email address below. Find out more about saving to your Kindle.

Note you can select to save to either the @free.kindle.com or @kindle.com variations. ‘@free.kindle.com’ emails are free but can only be saved to your device when it is connected to wi-fi. ‘@kindle.com’ emails can be delivered even when you are not connected to wi-fi, but note that service fees apply.

Find out more about the Kindle Personal Document Service.

Available formats
×

Save book to Dropbox

To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Dropbox.

Available formats
×

Save book to Google Drive

To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Google Drive.

Available formats
×